Database ni mkusanyiko wa taarifa zilizopangwa vizuri na kuhifadhiwa kwa njia ya kielektroniki ili ziweze kupatikana, kusomwa, kuongezwa au kufutwa kwa urahisi. Database hutumika katika programu nyingi kama mifumo ya shule, hospitali, benki, maduka na hata mitandao ya kijamii.

Mfumo wa database husaidia katika kutunza taarifa kama majina ya wanafunzi, malipo ya wateja, hesabu za bidhaa, na rekodi nyingine muhimu. Lugha maarufu ya kuwasiliana na database ni SQL (Structured Query Language).

Mifano ya Database Maarufu:

MySQL – hutumika sana kwenye PHP na WordPress.

Oracle – hutumiwa na mashirika makubwa.

MongoDB – database isiyo na muundo wa jedwali (NoSQL).

Microsoft SQL Server – hutumiwa katika mifumo ya kampuni kubwa.

Firebase – hutumiwa katika apps za simu.